Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI JAFO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA JENGO LA OFISI ZA TBS JIJINI DODOMA


WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akikagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.

Na.Gideon Gregory,-DODOMA

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo ametoa maagizo kwa Taasisi zake zote kutumia bidhaa za ndani za ujenzi na kupiga marufuku uagizwaji wa vifaa hivyo nje ya nchi.

Waziri Dkt. Jafo ameyasema hayo leo Julai 19,2024 Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kukagua na kuona maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Shirika la Viwango Tanzania (TBS) huku akisisitiza kuwa ujenzi wowote utakao anza vifaa vinunuliwe ndani ya nchini.

"Vipo viwanda vikubwa ndani ya nchi viwanda hivyo badala ya kuzalisha China wameamua kuja kuzalisha Tanzania na vinamasoko Kenya Burundi, Uganda na Kongo sasa ninavyosikia jengo limechelewa kwa kuagiza vioo nchini China nawashangaa, " amesema Dkt. Jafo.

Waziri Jafo ameridhishwa na kazi inayoendelea na matarajio ifikapo Oktoba 15,2024 ujenzi uwe umekamilika.


"Kwa kweli nawapongeza kwa ujenzi huo wa jengo kwani linaendana na thamani ya fedha iliyotolewa na Serikali ya shilingi bilioni 24."amesema

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw.Needpeace Wambuya, amesema kwa ujezi wa jengo hilo unakwenda kusogeza huduma ya haraka kwa upimaji ubora wa bidhaa kwa wadau lakini pia wamechukua maelekezo bidhaa zote zinatumika za hapa nchini.

"Tasisi zilizopo chini ya wizara wizara ziwe mfano kuhakikisha bidhaa zote zinazotumika kwenye ujenzi zinatoka ndani ya nchi kwa kulinda viwanda vetu, ajira na tupunguze fedha za kigeni, " amesema Bw.Wambuya

Naye Meneja wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya kati, Nickonia Mwambuka ameshukuru kwa ziara hiyo ya Waziri na kuahidi kuwa hadi kufikia Oktoba 15,2024 Jengo hilo litakuwa limekamilika na watafanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu ili jengo hilo likamilike kwa wakati.

"Pia watalifanyia kazi suala maabala kwani ujenzi huo wa maabala utasaidia mikoa ya Kanda ya kati wajasiriamli na wafanyabishara itakuwa rahisi kuchukua sampuli kupimwa na kupata majibu kwa wakati",amesema.

Hata hivyo Ujezi wa jengo Hilo la TBS linathamani ya shilingi billioni 24.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akizungumza na wadhibiti ubora wakati alipotembelea Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) leo Julai 19,2024 jijini Dodoma.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akikagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akitoa maelezo wakati akikagua Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akizungumza mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.



WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo,akizungumza mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw.Needpeace Wambuya,akizungumza mara baada ya Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo (hayupo pichani) mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.




Meneja wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya kati, Nickonia Mwambuka,akimpongeza Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt, Selemani Jafo (hayupo pichani) mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.


Muonekano wa Ujenzi wa Jengo la Ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lililopo eneo la Njedengwa, jijini Dodoma,leo Julai 19,2024.

Post a Comment

0 Comments