Ticker

6/recent/ticker-posts

KATIBU MKUU NISHATI ATEMBELEA BANDA LA EWURA MAONESHO YA NANENANE DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio wakimsikiliza Meneja wa Kanda ya kati Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Bi.Hawa Lweno,walipotembelea Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba,akizungumza kwenye banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) alipotembelea Banda hilo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba,akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio wakifurahi mara baada ya kukabidhiwa zawadi ya mifuko ya EWURA walipotembelea banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Meneja wa Kanda ya kati Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Bi.Hawa Lweno,akitoa elimu kwa wanafunzi waliofika katika Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.

Post a Comment

0 Comments